Local, Normal News, Taifa Stars, Yanga

Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2d ago
Gamondi ateta na viongozi, benchi la ufundi Yanga

Kocha Mkuu wa Timu ya Taifa ya Tanzania, Taifa Stars, Miguel Gamondi, ameendelea na ziara yake ya kutembelea klabu za Ligi Kuu ya NBC, ambapo leo ametembelea Klabu ya Yanga.

Ziara hiyo inalenga kuimarisha ushirikiano kati ya timu za Taifa na klabu, pamoja na kubadilishana mawazo kuhusu namna ya kuboresha maendeleo ya soka nchini.

Gamondi alipata nafasi ya kufanya mazungumzo na viongozi wa Yanga pamoja na benchi la ufundi la klabu hiyo, katika kikao kilicholenga kujenga uhusiano wa karibu na kuweka mazingira bora ya ushirikiano kati ya Taifa Stars na klabu.

Kocha Mkuu wa Yanga, Manqoba Mngqithi, alishiriki katika kikao hicho akiwa ameambatana na baadhi ya maafisa wa benchi la ufundi pamoja na viongozi wa klabu.

Ziara hiyo ya Gamondi inatarajiwa kuwa sehemu muhimu katika kuhakikisha Taifa Stars inapata ushirikiano wa karibu na klabu, hasa katika masuala ya maendeleo ya wachezaji, maandalizi ya timu na kuboresha ushindani wa soka la Tanzania.

Kwa upande wa Yanga, kikao hicho kimetoa fursa kwa pande zote mbili kubadilishana uzoefu na mawazo, huku kikiweka msingi wa ushirikiano zaidi kati ya klabu hiyo na timu ya Taifa.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
8h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
10h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
12h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
13h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
15h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’