Local, Normal News, Simba Sc

Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea

Joel JJ By Joel JJ
β€’
2d ago
Doumbia akiri mambo magumu, haijawahi kutokea

Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Doumbia, amekiri kuwa anapitia kipindi kigumu cha kutofunga mabao katika hatua za mwanzo za msimu, akisema hali hiyo ni jambo jipya kwake tangu aanze kucheza soka la ushindani.

Doumbia amesema licha ya kupata nafasi za kucheza, bado hajafanikiwa kufungua akaunti yake ya mabao, hali ambayo amesema haijawahi kumkuta katika hatua kama hii ya msimu.

“Ni mara ya kwanza kabisa kwangu kupitia kipindi cha aina hii, kwa sababu hii ni ligi ambayo ndiyo kwanza imeanza. Kwa hiyo ni jambo la kawaida, hasa unapokuwa unapata nafasi yako ya kwanza. Hivyo, hii ni mara yangu ya kwanza kupitia hali kama hii,” amesema Doumbia.

Hata hivyo, mshambuliaji huyo anaendelea kupata sapoti kutoka kwa mashabiki wa Simba, huku benchi la ufundi chini ya kocha Steve Barker likionyesha imani kwake licha ya changamoto hiyo ya kufunga.

Doumbia pia ameendelea kuonyesha dalili za uwezo wake kila anapopewa nafasi. Katika dakika chache alizocheza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mighty Wanderers, mshambuliaji huyo alionyesha ubora na uwezo wa kuleta tofauti katika safu ya ushambuliaji.

Kwa sasa, kinachosubiriwa ni Doumbia kupata bao lake la kwanza, ambalo linaweza kuwa mwanzo wa kuondoa presha na kumfungulia njia ya kurejea kwenye kiwango ambacho mashabiki wa Simba wanakitarajia kutoka kwake.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
6h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
10h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
16h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
18h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
22h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’