Local, Normal News, Yanga SC, Sele Day

Yanga yatangaza “Sele Day” kumkaribisha Selemani Mwalimu Jangwani

Jairo Mtitu By Jairo Mtitu
3d ago
Yanga yatangaza “Sele Day” kumkaribisha Selemani Mwalimu Jangwani

Yanga SC imeandaa siku maalum ya kumkaribisha mshambuliaji wake Selemani Mwalimu, ambapo mchezo ujao wa timu hiyo umetangazwa kuwa “Sele Day” kwa ajili ya kumpa mapokezi ya kipekee nyota huyo.

Akizungumza kuhusu mpango huo, mmoja wa viongozi na wanachama wa Yanga, Alikamwe, amesema mchezo huo umetengwa maalum kwa ajili ya kumkaribisha Selemani Mwalimu baada ya kujiunga na klabu hiyo.

Amesema siku hiyo itakuwa ya kipekee kwa Wananchi, huku akiwataka mashabiki kushiriki katika maandalizi ya kumpokea mchezaji huyo kwa namna ya pekee.

“Siku ya mchezo huu tumei-Dedicate kwa mchezaji wetu Selemani Mwalimu na itakuwa Sele Day. Ni siku maalumu ya kumkaribisha Selemani Mwalimu Jangwani na kwa kuwa amefanya jambo la kimpira kule Botswana, basi Wananchi tunataka kumkaribisha vizuri.”

Katika kuongeza hamasa kuelekea siku hiyo, Alikamwe pia ametoa wito wa kipekee kwa mashabiki wa Yanga, akiwahimiza kuchagua sehemu moja ya mwili yenye nywele na kuweka bleach, kisha kutuma picha zao kama sehemu ya maandalizi ya “Sele Day.”

Mpango huo unatarajiwa kuongeza shangwe miongoni mwa mashabiki wa Yanga na kufanya siku hiyo kuwa ya kipekee kwa Selemani Mwalimu pamoja na Wananchi watakaofika uwanjani.

Kwa sasa, hamasa imeanza kujengwa kuelekea mchezo huo, huku mashabiki wa Yanga wakisubiri kwa hamu kumpokea rasmi Selemani Mwalimu Jangwani.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
5h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
8h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
10h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
12h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
14h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
15h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
15h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
17h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
20h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →