International, Normal News, Tevez, Messi, Ronaldo, Argentina, Manchester united,

Tevez kuvunja mwiko, Messi na Ronaldo kucheza timu moja

Abdulrahman Said By Abdulrahman Said
β€’
4d ago
Tevez kuvunja mwiko, Messi na Ronaldo kucheza timu moja

Mchezaji wa zamani wa Manchester United na Juventus, Carlos Tévez, anapanga kufanya mchezo wake wa kuaga soka katika Uwanja wa La Bombonera, Argentina, mwezi Desemba 2026, miaka minne baada ya kutangaza kustaafu rasmi.

Katika mchezo huo, Tévez anatarajia kuwaalika baadhi ya mastaa aliowahi kucheza nao, huku Lionel Messi na Cristiano Ronaldo wakiwa miongoni mwa majina makubwa anayataka yashiriki katika tukio hilo. Tévez anataka kuwaona nyota hao wakicheza upande mmoja katika mchezo huo maalum.

Tévez amesema kuwa kuwaunganisha Messi na Ronaldo katika timu moja ni ndoto yake ya muda mrefu, akiamini tukio hilo litakuwa la kipekee kwa mashabiki wa soka duniani. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa, nyota hao wawili tayari wamekubali kushiriki katika mchezo huo.

Tévez alicheza pamoja na Ronaldo akiwa Manchester United na Messi katika Timu ya Taifa ya Argentina. Pia aliitumikia Boca Juniors katika vipindi mbalimbali, akicheza jumla ya mechi 279 na kufunga mabao 94, huku La Bombonera ikiwa moja ya viwanja vyenye umuhimu mkubwa katika historia yake ya soka.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
7h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
11h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
12h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
14h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
16h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
17h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
17h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
19h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’