International, Transfer News, Ac Milan, Aston Villa

Rafael Leão Ajiunga na Aston Villa kwa Mkopo.

Xtra 90 Media By Xtra 90 Media
28 Aug 2026
Rafael Leão Ajiunga na Aston Villa kwa Mkopo.

Aston Villa imekamilisha dili la kumsajili winga wa kimataifa wa Ureno, Rafael Leão, kutoka AC Milan kwa mkopo. Kwa mujibu wa taarifa hiyo, makubaliano yamefikia hatua ya mwisho na nyaraka zote za uhamisho tayari zimekamilishwa, hivyo Leão sasa anajiandaa kuanza ukurasa mpya wa maisha yake ya soka akiwa England.

Katika dili hilo, Aston Villa imepata nafasi ya kumnunua moja kwa moja Leão kupitia kipengele cha buy option chenye thamani ya takribani pauni milioni 41. Hii inamaanisha kuwa baada ya kipindi cha mkopo, Villa inaweza kutumia fursa hiyo kumsajili mshambuliaji huyo kwa mkataba wa kudumu iwapo atafanya vizuri na klabu ikaamua kuendelea naye.

Aston Villa pia imekubali kubeba mshahara wa Leão unaokadiriwa kufikia euro milioni 8 kwa mwaka. Kocha Unai Emery ametajwa kuwa mtu muhimu katika kufanikisha uhamisho huo, akiongoza kwa karibu jitihada za klabu hiyo kumpata winga huyo ambaye anajulikana kwa kasi, uwezo wa kupiga chenga na kutengeneza nafasi pamoja na kufunga mabao.

Kwa Aston Villa, ujio wa Leão ni nyongeza kubwa katika safu ya ushambuliaji na unaonyesha wazi dhamira ya klabu hiyo kujenga kikosi chenye ushindani zaidi. Kwa upande wa Leão, uhamisho huu unampa nafasi ya kujaribu changamoto mpya katika Premier League baada ya kipindi chake AC Milan. Sasa macho yote yatakuwa kwake kuona kama ataweza kuonyesha kiwango kikubwa ndani ya kikosi cha Unai Emery na hatimaye kuifanya Aston Villa iamue kutumia pauni milioni 41 kumnunua moja kwa moja.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE →
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
5h ago
READ MORE →
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE →
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE →
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: João Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE →
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE →
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE →
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE →
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE →
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE →