Local, Transfer News, Simba Sc, Mashujaa, JKT

Simba kufunga dirisha la usajili na watatu

Joel JJ By Joel JJ
β€’
15 Aug 2026
Simba kufunga dirisha la usajili na watatu

Klabu ya Simba SC inatajwa kukamilisha usajili wa wachezaji watatu wapya, huku uongozi wa Wekundu wa Msimbazi ukiharakisha kukamilisha mipango hiyo kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili usiku wa leo Jumamosi, August 15 2026

Miongoni mwa wachezaji wanaotarajiwa kutua Msimbazi ni mshambuliaji wa JKT Tanzania, Paul Peter Kasunda, mwenye umri wa miaka 27. Kasunda tayari amefikia makubaliano binafsi na Simba, huku klabu hiyo ikimalizia mazungumzo na JKT Tanzania kabla ya kumtambulisha rasmi.

Mshambuliaji huyo anatarajiwa kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji ya Simba baada ya kufanya vizuri msimu uliopita, ambapo aliifungia JKT Tanzania mabao nane.

Simba imeamua kumfuata Kasunda baada ya kushindikana kwa mpango wa kumsajili mshambuliaji Pape Abdou N’diaye, ambaye klabu yake haikuwa tayari kumuuza katika kipindi hiki.

Mbali na Kasunda, Simba tayari imekamilisha usajili wa Ibrahim Nindi, beki wa kati mwenye umri wa miaka 18, aliyekuwa akiitumikia KMC msimu uliopita. Nindi amejiunga na Simba kwa mkataba wa miaka mitatu akiwa mchezaji huru baada ya kumaliza mkataba wake na KMC.

Nindi ana historia ya kuifahamu Simba, kwani alilelewa katika kikosi cha vijana cha Simba U20 kabla ya kujiunga na Mashujaa FC na baadaye KMC. Pia amewahi kuitumikia Singida Black Stars katika michuano ya CECAFA Kagame Cup.

Usajili wa Nindi unaonekana kuwa sehemu ya mkakati wa Simba wa kujenga kikosi chenye vijana wenye uwezo wa kuitumikia klabu kwa muda mrefu.

Mchezaji mwingine ambaye tayari ametua Msimbazi ni Ismail Mgunda, aliyesajiliwa kutoka Mashujaa FC. Hivyo, Simba imekuwa ikifanya usajili wa haraka katika siku za mwisho za dirisha.

More Stories

APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
APR Fc yawaondosha aigles du congo kwenye caf champions league
2h ago
READ MORE β†’
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
Azam Fc yaomboleza kifo cha mlinda lango U20
6h ago
READ MORE β†’
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
Hatuna presha kuikabili Yanga - Kocha Gaborone United
7h ago
READ MORE β†’
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
Manqoba aweka tahadhari mechi dhidi ya Gaborone United
9h ago
READ MORE β†’
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
Rasmi: JoΓ£o Pedro Atwaa Tuzo Ya Mchezaji Bora Wa Mwezi Wa Agosti
11h ago
READ MORE β†’
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
Simba inalenga hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika, nusu fainali ni lengo kubwa
12h ago
READ MORE β†’
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
Libasse awapiga chini Max na Mwajanga, Kwenye tuzo za Mwezi.
12h ago
READ MORE β†’
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
Fei Toto azipotezea Simba, Yanga
14h ago
READ MORE β†’
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
Xtra 90 Bets : Utabiri wa mechi 21, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
UEFA champions league: matokeo ya usiku
UEFA champions league: matokeo ya usiku
1d ago
READ MORE β†’