Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' leo inaanza kampeni ya kuwania tiketi ya michuano ya Afcon 2025 kwa kuikabili Ethiopia katika mchezo wa kundi H utakaopigwa saa 1 usiku
Ili kujiweka katika nafasi nzuri, Stars inapaswa kuhakikisha inashinda mechi zote tatu za nyumbani wakianza na Ethiopia leo
Katika makaratasi, ni mechi ambayo Stars inapaswa kushinda kwa kuangalia viwango na ubora wa timu zote kwa wakati huu
Hata hivyo ni mechi ambayo wachezaji wa Taifa Stars hswapaswi kudharau, badala yake wanapaswa kwenda kupambana ili kupata matokeo mazuri
Kikosi cha Stars leo kitashuka dimbani bila ya nyota wake Mbwana Samatta na Saimon Msuva ambao hawakujumuishwa katika kikosi
Hata hivyo nyota hao pia hawakujumuishwa katika mechi iliyopita ya kuwania kufuzu kombe la Dunia dhidi ya Zambia na Stars kuibuka na ushindi wa bao 1-0 ugenini



