Mpya

Pacome bado anaisubiri tuzo ya MVP 2024/25

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
β€’
2d ago
Pacome bado anaisubiri tuzo ya MVP 2024/25

Kiungo mshambuliaji wa kimataifa wa Yanga, Pacome Zouzoua, bado anasubiri tuzo ya Mchezaji Bora (MVP) wa msimu wa 2024/25, ambayo anaamini alistahili kuipata iicha ya ukimya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF).

Msimu huo ulikwisha kwa Yanga kutetea ubingwa wao huku Pacome akiwa mhimili mkubwa wa mafanikio hayo. Hadi sasa sherehe za utoaji wa tuzo hizo kwa misimu miwili sasa hazijafanyika, jambo linalozua maswali mengi miongoni mwa wadau wa soka nchini.

Katika msimu huo, raia huyo wa Ivory Coast alionyesha kiwango cha hali ya juu ambapo alifanikiwa kufunga mabao 11 na kutoa pasi 9 akiibeba Yanga kutetea taji la ligi kuu mwa msimu wa nne.

Pacome alifunga bao la kwanza kwenye mchezo wa mwisho kuhitimisha msimu dhidi ya Simba huku akitoa pasi ya bao la pili lililofungwa na Clement Mzize katika mchezo ambao Yanga iliibuka na ushindi wa mabao 2-0.

Akizungumza jana nyumbani kwake baada ya kutembelewa na Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe, Pacome alitumia nafasi hiyo kuuliza vipi mpaka sasa tuzo hizo hazijatolewa pengine akitarajia wahusika kutoa ufafanuzi juu ya mkwamo uliopo.

More Stories

Toure anajiamini, atafunga sana
Toure anajiamini, atafunga sana
3h ago
READ MORE β†’
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
6h ago
READ MORE β†’
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
6h ago
READ MORE β†’
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
6h ago
READ MORE β†’
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
9h ago
READ MORE β†’
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
10h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
13h ago
READ MORE β†’
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
1d ago
READ MORE β†’
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
1d ago
READ MORE β†’