Mpya

Yanga yasaini Mkataba wa Ujenzi wa Yanga Tower

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
β€’
2d ago
Yanga yasaini Mkataba wa Ujenzi wa Yanga Tower

Klabu ya Yanga imeandika sura mpya katika historia yake baada ya kusaini rasmi mkataba wa ujenzi wa jengo la kisasa la kibiashara, Yanga Tower, litakalojengwa katika eneo la Kariakoo, Dar es Salaam.

Akizungumza wakati wa hafla ya utiaji saini, Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, amesema mradi huo ni utekelezaji wa maono ya muda mrefu ya wazee wa klabu hiyo, ambao tangu miaka ya 1960 walitamani kuwa na jengo litakalokuwa makao na chanzo cha shughuli za taasisi.

Injinia Hersi amesema juhudi za kupata eneo hilo zilihusisha hata klabu kucheza mechi za kirafiki na kutumia mapato ya milangoni kusaidia kununua ardhi hiyo. Miongoni mwa mechi hizo ilikuwa dhidi ya klabu ya Leopards ya Kenya, hatua ambayo inaendelea kuwa sehemu muhimu ya historia ya Yanga.

“Leo sisi tumebeba jukumu la kuendeleza maono hayo. Tunapoanza safari hii ya ujenzi hatujengi tu jengo, tunajenga historia, tunajenga urithi na tunajenga kwa ajili ya vizazi vijavyo,” alisema Hersi.

Mkataba wa Shilingi Bilioni 5.5

Ujenzi wa Yanga Tower utatekelezwa na Group Six International, kampuni iliyopatikana baada ya mchakato wa zabuni na tathmini ya uwezo, ubora wa kazi, gharama na muda wa utekelezaji.

Mkataba huo una thamani ya Shilingi bilioni 5.5, huku mradi ukitarajiwa kukamilika ndani ya takribani miezi 12.

Jengo hilo litakuwa na matumizi mchanganyiko, likiwa na maeneo ya biashara katika basement, ground floor na first floor, huku ghorofa ya pili hadi ya kumi zikitumika kama maghala ya kuhifadhi bidhaa.

Ghorofa ya 11 na 12 zitatengwa kwa ajili ya makazi, zikiwa na takribani units 13, wakati rooftop itakuwa eneo la kijamii litakalotumika kwa mapumziko, kahawa na chakula, mikutano pamoja na kutazama michezo.

Kwa muundo huo, Yanga Tower inalenga kuwa zaidi ya jengo la klabu, bali kituo cha biashara, makazi na shughuli za kijamii katikati ya Kariakoo.

Azania Bank Yatoa Ufadhili

Katika hatua nyingine muhimu, Azania Bank ndiyo benki itakayofadhili ujenzi wa mradi huo kwa kiasi cha Shilingi bilioni 5.5.

Mkurugenzi wa Mali na Miamala wa Azania Bank, Eugene Kimaro, amesema benki hiyo inaamini katika maono ya Yanga na iko tayari kuhakikisha fedha za mradi zinapatikana na utekelezaji unafanyika kama ulivyopangwa.

“Nimpongeze sana Injinia Hersi kwa maono yake ya kuifanya klabu hii kuwa ya mfano katika kila idara. Ndani ya miezi 12 tunatarajia kurejea hapa kwa ajili ya kuzindua jengo hili,” alisema Kimaro.

Kwa upande wake, Group Six kupitia QS Leon, imeahidi kuzingatia mambo matatu makuu katika utekelezaji wa mradi huo: thamani ya fedha, ubora wa kazi na muda.

More Stories

Toure anajiamini, atafunga sana
Toure anajiamini, atafunga sana
3h ago
READ MORE β†’
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
6h ago
READ MORE β†’
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
6h ago
READ MORE β†’
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
6h ago
READ MORE β†’
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
9h ago
READ MORE β†’
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
10h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
13h ago
READ MORE β†’
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
1d ago
READ MORE β†’
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
1d ago
READ MORE β†’