Mpya

Yanga yatangaza viingilio 'Sele Day'

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
β€’
3d ago
Yanga yatangaza viingilio 'Sele Day'

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe ametangaza viingilio vya mchezo wa ligi ya mabingwa kati ya Yanga dhidi ya Gaborone United utakaopigwa Jumamosi, Septemba 12 katika uwanja wa Azam Complex.

Mchezo huo maalum 'Sele Day' unatarajiwa kupigwa kuanzia saa 1 usiku Kamwe akiwataka Wananchi kujitokeza kwa wingi kuiunga mkono timu yao.

"Viingilio vya mchezo wa marudiano ligi ya mabingwa Afrika dhidi ya Gaborone United, VIP A ni Tsh 30,000/- , VIP B ni Tsh 10,000/- na Mzunguuko ni Tsh 5,000/-"

"Tiketi za mchezo huu zinapatikana kuptia N-Card na tayari zinapatikana kwenye mfumo niwaase mashabiki mchangamkie tiketi hizi mapema," alisema Kamwe.

Kamwe amesema kiungo mshambuliaji Pacome Zouzoua atakuwa sehemu ya watazamaji wa mchezo huo uwanja wa Azam Complex huku akieleza sababu ya mchezo huo kupewa mchezaji Seleman Mwalimu 'Gomez'.

"Tumeidediicate mechi hii kwa Seleman Mwalimu kwa sababu wakati tulipomsajili hatukupata muda wa kumtambulisha vyema. Na zaidi alifanya jambo kubwa pale Gaborone hivyo tunaona hii ni nafasi yetu Wanayanga kumkaribisha kijana wetu na kuwapa nguvu wachezaji wetu waone sisi wanachama na mashabiki tunasimama na timu yetu," alisema Kamwe

More Stories

Toure anajiamini, atafunga sana
Toure anajiamini, atafunga sana
3h ago
READ MORE β†’
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
6h ago
READ MORE β†’
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
6h ago
READ MORE β†’
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
6h ago
READ MORE β†’
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
9h ago
READ MORE β†’
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
10h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
13h ago
READ MORE β†’
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
1d ago
READ MORE β†’
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
1d ago
READ MORE β†’