Mpya

Pacome awatumia ujumbe wachezaji Botswana

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
β€’
5 Sep 2026
Pacome awatumia ujumbe wachezaji Botswana

Kiungo mshambuliaji wa Yanga Pacome Zouzoua, amewatumia ujumbe wa hamasa wachezaji na familia nzima ya Wananchi kuelekea kuanza kwa safari ya klabu hiyo katika Ligi ya Mabingwa Afrika.

Pacome, ambaye hatakuwa sehemu ya kikosi cha Yanga kwa sasa akiendelea kuuguza jeraha la mguu, amesema moyo na mawazo yake yako pamoja na timu katika kipindi hiki muhimu.

Kupitia ujumbe wake, nyota huyo amewataka wachezaji wa Yanga kupambana hadi dakika ya mwisho, wakicheza kwa kujituma na kuhakikisha wanaibeba vyema jezi ya klabu hiyo.

β€œBahati njema kwa familia nzima ya Yanga katika safari hii mpya ya Champions League. Kwa bahati mbaya, kutokuwepo kwangu kunanifanya nisiwe pamoja nanyi uwanjani, lakini moyo na mawazo yangu yako pamoja na timu.”

Pacome ameongeza kuwa anaamini uwezo wa kikosi hicho na ataendelea kuwaunga mkono hata akiwa mbali.

β€œToeni kila kitu, piganeni hadi mwisho na ifanyieni heshima jezi yetu. Ninawaamini na nitakuwa pamoja nanyi, hata kutoka mbali,” aliandika

Yanga inaanza safari yake ya ligi ya mabingwa leo kwa mchezo wa hatua ya awali dhidi ya Gaborone United utakaopigwa uwanja wa Taifa wa Botswana usiku wa leo saa 2 kwa saa za Tanzania

More Stories

Toure anajiamini, atafunga sana
Toure anajiamini, atafunga sana
3h ago
READ MORE β†’
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
Manqoba aondoka na tuzo ya ligi kuu August
6h ago
READ MORE β†’
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
Mwalimu awaalika Wananchi SELE DAY
6h ago
READ MORE β†’
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
Hatutawadharau Gaborone United - Manqoba
6h ago
READ MORE β†’
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
Aziz Ki apunguziwa presha Yanga
9h ago
READ MORE β†’
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
Sele Day tiketi zinaelekea ukingoni
10h ago
READ MORE β†’
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
Manqoba na ndoto ya fainali ligi ya mabingwa
10h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
13h ago
READ MORE β†’
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
Pacome aongoza hamasa KMC Complex
1d ago
READ MORE β†’
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
Media Day; Manqoba, Kamwe wafunguka mipango ya kuikabili Gaborone United
1d ago
READ MORE β†’