Alama tatu muhimu kwa Yanga zimefufua matumaini kwa Wananchi kufuzu robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Β
Ni baada ya ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya TP Mazembe katika mchezo uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Bao la dakika za mapema lililofungwa na Mazembe kupitia mkwaju wa penati lilikaribia kuvuruga furaha ya Wananchi lakini Clement Mzize akaweka mzani sawa kabla ya mapumziko akifunga bao la aina yake kutoka nje ya 18
Wanasema mechi kubwa zinawahitaji wachezaji wakubwa, ndivyo ilivyokuwa Stephane Aziz Ki akifunga bao la pili kabla ya Mzize kuongeza bao la tatu dakika chache baadae akimalizia kazi nzuri ya Prince Dube
Ilikuwa mechi muhimu kwa Yanga kuibuka na ushindi alama hizi tatu zinafufua matumaini ya kufuzu robo fainali
Yanga imesogea nafasi ya tatu, baada ya kufikisha alama nne
Mchezo unaofuata ni ugenini dhidi ya AL HILAL , Januari 12
ITAWEZEKANA.....!