Legal Director of the Yanga club Simon Patrick has supported the statement made in Parliament today by Hon. George Simbachawene, Minister Office of the President - Management of Public Service and Good Governance that if Simba Sc has evidence of some of players being bribed leading to a 5-1 defeat from Yanga, then it is better that they file their complaint to the office of TAKUKURU
"Kwa mujibu wa kifungu na. 15 cha sheria na. 329, kama ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2022, kinasema kutoa na kupokea rushwa ni kosa la jinai na adhabu yake ni faini pamoja na kifungo kuanzia miaka 3 mpaka 5.
Kama mnahisi kuna wachezaji au viongozi walipokea rusha, ni vyema kufuata ushauri wa Mh. Simbachawene leo Bungeni kwenda ofisi za TAKUKURU - Temeke kufungua kesi, kisha kuiandikia TFF na FIFA ili hatua kali zichukuliwe kwa maendeleo ya mpira wetu.
Lakini kumbukeni, kumtuhumu mtu kwa kosa kubwa kama hilo bila ushahidi adhabu yake unaweza kuishia kulipa mabilioni ya fedha kwa reputation damage.
Ushauri wa bure, nendeni mkafungue kesi kama mna ushahidi, kinyume na hapo jipangeni upya mpira ni mchezo wa wazi, nyie sio timu ya kwanza kupigwa 5G msimu huu.
Haiwezekani wachezaji wa kuteka Airport waje wapambane na wachezaji waliofanyiwa scouting!"