Mpya

Mechi za Yanga kuambatana na burudani mbalimbali

Shabiki NambaMoja By Shabiki NambaMoja
β€’
26 Oct 2021
Mechi za Yanga kuambatana na burudani mbalimbali

Msemaji wa Yanga Haji Manara amesema mchezo dhidi ya Azam Fc ambao utapigwa Jumamosi, Oktoba 30 kwenye uwanja wa Benjamin Mkapa, utaambatana na burudani mbalimbali

Manara amesema kama klabu wamekuja na utaratibu wa kuzifanya mechi zote wanazocheza nyumbani kuwa sehemu ya burudani kwa mashabiki wao

Jumamosi kabla ya mchezo kutakuwa na burudani za utangulizi kutoka kwa wasanii mbalimbali, utaratibu ambao wataufanya kwa michezo yote wanayocheza nyumbani

"Tunataka mechi zetu iwe sehemu ya burudani, mashabiki wanapotoka nyumbani kuja uwanjani, watakuwa wakipata burudani mbalimbli kabla ya mchezo. Barani Ulaya jambo hili wanafanya nasi tumeona si vibaya kulianzisha kwa kuanzia Jumamosi kwenye mchezo dhidi ya Azam," alisema Manara

"Kutakuwa na burudani kutoka kwa wasanii mbalimbali ambao majina yao tutayatangaza, lengo ni kuifanya siku hiyo shabiki aweze kutoka kwake na familia yake kufuata burudani kama tunavyofanya kwenye wiki ya Mwananchi"

Akizungumzia mchezo dhidi ya Azam Fc, Manara amesema mshindani wao halisi katika mbio za ubingwa msimu huu ni Azam Fc hivyo wanawaheshimu

Lakini amesema Yanga imejipanga kushinda ubingwa hivyo watahakikisha wanaondoka na alama zote tatu

More Stories

Yanga Complete Preparations Ahead of Gaborone United CAF Champions League Clash
Yanga Complete Preparations Ahead of Gaborone United CAF Champions League Clash
4h ago
READ MORE β†’
Toure Confident His Goals Will Come as He Adapts to Life at Yanga
Toure Confident His Goals Will Come as He Adapts to Life at Yanga
8h ago
READ MORE β†’
Mngqithi Named NBC Premier League Coach of the Month for August
Mngqithi Named NBC Premier League Coach of the Month for August
11h ago
READ MORE β†’
Gomez Calls on Yanga Fans to Fill Azam Complex Ahead of Gaborone United Decider
Gomez Calls on Yanga Fans to Fill Azam Complex Ahead of Gaborone United Decider
11h ago
READ MORE β†’
Mngqithi Warns Yanga Against Complacency Ahead of Gaborone United Decider
Mngqithi Warns Yanga Against Complacency Ahead of Gaborone United Decider
12h ago
READ MORE β†’
Mngqithi Reveals Aziz Ki’s Fitness Limit Ahead of Gaborone United Return Leg
Mngqithi Reveals Aziz Ki’s Fitness Limit Ahead of Gaborone United Return Leg
14h ago
READ MORE β†’
Yanga Fans Snap Up Tickets Ahead of Gaborone United Decider
Yanga Fans Snap Up Tickets Ahead of Gaborone United Decider
15h ago
READ MORE β†’
Mngqithi Believes Yanga Can Reach CAF Champions League Final
Mngqithi Believes Yanga Can Reach CAF Champions League Final
16h ago
READ MORE β†’
Today's Newspapers, Friday, September 11, 2026
Today's Newspapers, Friday, September 11, 2026
18h ago
READ MORE β†’
Pacome Visits Yanga Teammates as He Continues Recovery from Injury
Pacome Visits Yanga Teammates as He Continues Recovery from Injury
1d ago
READ MORE β†’