Mpya

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
7h ago
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru

Kikosi cha Simba leo kimefanya mazoezi kwenye uwanja wa Uhuru kuelekea mchezo wa mkondo wa pili hatua ya awali ligi ya mabingwa dhidi ya Mighty Wonderers. Mchezo huo utapigwa siku ya Jumapili, Septemba 13 katika uwanja huo.

Vijana wa kocha Steve Barker wamekamilisha mazoezi yao katika uwanja huo kwani kesho kikosi kinatarajiwa kufanya mazoezi ya mwisho kwenye uwanja wake wa Mo Simba Arena huku Mighty Wonderers wakitarajiwa kufanya mazoezi katika dimba la Uhuru saa 10 jioni kwa mujibu wa kanuni.

Dimba la Uhuru limefanyiwa maboresho makubwa hasa katika eneo la kuchezea 'pitch' hivyo kuwapa nafasi nzuri Wana Lunyasi kuweka soka chini katika mchezo ambao Wekundu wa Msimbazi watahitaji ushindi au matokeo yoyote ya sare kutinga hatua inayofuata.

Wapinzani wao Mighty Wonderers tayari wamewasili nchini ambapo timu hiyo iliwasili Alhamisi usiku.

Mchezo baina ya timu hizo utapigwa Jumapili saa 10 jioni..

More Stories

Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
10h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
14h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
14h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’