Mpya

Libasse amemaliza adhabu CAF, Kapombe bado - Ahmed

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
2d ago
Libasse amemaliza adhabu CAF, Kapombe bado - Ahmed

Klabu ya Simba imethibitisha kuwa kiungo wake, Libasse Geye, amemaliza adhabu yake ya kadi nyekundu katika mashindano ya CAF na anaruhusiwa kurejea kwenye kikosi kitakachokutana na Mighty Wanderers katika mchezo wa marudiano wa Ligi ya Mabingwa Afrika.

Akizungumza, Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba, Ahmed Ally, amesema Libasse alimaliza adhabu yake baada ya kukosa mechi mbili za Ligi ya Mabingwa Afrika, huku beki Shomari Kapombe akiwa bado anapaswa kutumikia adhabu yake.

Libasse alionyeshwa kadi nyekundu baada ya mchezo dhidi ya Petro de Luanda uliochezwa Februari 7, 2026 nchini Angola na kumalizika kwa sare ya bao 1-1. Ahmed amesema tukio hilo lilitokea baada ya mchezo kumalizika, tofauti na Kapombe ambaye alitolewa wakati mchezo ukiendelea.

Kwa mujibu wa Ahmed, tukio lililosababisha kadi hiyo lilihusisha pia mchezaji wa Simba, Alassane Kante, lakini waamuzi walimchukulia hatua Libasse.

Kutokana na adhabu hiyo, Libasse alikosa michezo miwili ya Ligi ya Mabingwa Afrika; dhidi ya Stade Malien katika msimu wa 2025/26 na dhidi ya Mighty Wanderers katika hatua ya kwanza ya msimu wa 2026/27.

Hivyo, kurejea kwa Libasse kunampa Simba chaguo jingine muhimu katika eneo la kiungo wakati timu hiyo ikijiandaa kwa mchezo wa marudiano dhidi ya Mighty Wanderers.

Kwa upande mwingine, Kapombe ambaye pia ni majeruhi, bado hajaimaliza adhabu yake ya kukosa mechi tatu, hivyo atawakosa Mighyty Wonderers

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
8h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
11h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
15h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
15h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
18h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’