Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Doumbia, amekiri kuwa anapitia kipindi kigumu cha kutofunga mabao katika hatua za mwanzo za msimu, akisema hali hiyo ni mpya kwake tangu aanze kucheza soka la ushindani.
Doumbia amesema licha ya kupata nafasi za kucheza, bado hajafanikiwa kupata bao, jambo ambalo amelitaja kuwa sehemu ya changamoto za mchezo wa soka, hasa msimu unapokuwa umeanza.
“Ni mara ya kwanza kabisa kwangu kupitia kipindi cha aina hii, kwa sababu hii ni ligi ambayo ndiyo kwanza imeanza. Kwa hiyo ni jambo la kawaida, hasa unapokuwa unapata nafasi yako ya kwanza. Hivyo, hii ni mara yangu ya kwanza kupitia hali kama hii,” amesema Doumbia.
Doumbia anaamini hali hiyo ni sehemu ya mchakato wa msimu na kwamba kupata nafasi za kufunga ni hatua muhimu kabla ya mabao kuanza kupatikana.
Kauli ya Doumbia inakuja wakati Wanasimba wakiendelea kump sapoti huku benchi la ufundi chini ya kocha Steve Barker akionyesha kuwa na imani nae licha ya changamoto inayomkabili.
Licha ya kutofunga, Doumbia anaonekana kuwa ni mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa akidhihirisha hilo dakika chache alizocheza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mighty Wonderers.