Mpya

Doumbia akiri anapitia wakati mgumu

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
2d ago
Doumbia akiri anapitia wakati mgumu

Mshambuliaji wa Simba, Ibrahim Doumbia, amekiri kuwa anapitia kipindi kigumu cha kutofunga mabao katika hatua za mwanzo za msimu, akisema hali hiyo ni mpya kwake tangu aanze kucheza soka la ushindani.

Doumbia amesema licha ya kupata nafasi za kucheza, bado hajafanikiwa kupata bao, jambo ambalo amelitaja kuwa sehemu ya changamoto za mchezo wa soka, hasa msimu unapokuwa umeanza.

“Ni mara ya kwanza kabisa kwangu kupitia kipindi cha aina hii, kwa sababu hii ni ligi ambayo ndiyo kwanza imeanza. Kwa hiyo ni jambo la kawaida, hasa unapokuwa unapata nafasi yako ya kwanza. Hivyo, hii ni mara yangu ya kwanza kupitia hali kama hii,” amesema Doumbia.

Doumbia anaamini hali hiyo ni sehemu ya mchakato wa msimu na kwamba kupata nafasi za kufunga ni hatua muhimu kabla ya mabao kuanza kupatikana.

Kauli ya Doumbia inakuja wakati Wanasimba wakiendelea kump sapoti huku benchi la ufundi chini ya kocha Steve Barker akionyesha kuwa na imani nae licha ya changamoto inayomkabili.

Licha ya kutofunga, Doumbia anaonekana kuwa ni mshambuliaji mwenye uwezo mkubwa akidhihirisha hilo dakika chache alizocheza kwenye mchezo uliopita dhidi ya Mighty Wonderers.

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
13h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
16h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
19h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
20h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
23h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’