Mpya

Simba yaweka malengo ya fainali CAFCL

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
2d ago
Simba yaweka malengo ya fainali CAFCL

Mwenyekiti wa Kamati ya mashindano ya Simba, Swedi Mkwabi amewaita mashabiki wa Simba kuujaza uwanja wa Uhuru siku ya jumapili Septemba 13, 2026 itakapocheza mchezo wa marudiano dhidi ya Mighty Wanderes CAFCL.

Akizungumza muda mfupi baada ya kikosi cha Simba kurejea jijini Dar es salaam wakitokea Malawi, Mkwabi amesema ushindi waliopata ugenini ni matokeo muhimu ambayo yanawaweka katika nafasi nzuri ya kusonga mbele.

Hata hivyo jukumu la kila Mwana Simba ni kuhakikisha wanatimiza malengo yao kwenye mchezo wa marudiano uwanja wa Uhuru.

"Ulikuwa mchezo mgumu lakini ushindi yalikuwa matokeo muhimu sana kwetu. Tumerejea nyumbani, tutajiandaa vyema kwa ajili ya mchezo wa marudiano"

"Tunawaomba mashabiki wetu waje kwa wingi uwanja wa Uhuru siku ya Jumapili ili kuhakikisha tunakwenda kutimiza malengo yetu pamoja," alisema Mkwabi.

Aidha baada ya Simba kucheza hatua ya robo fainali mara kadhaa, Mkwabi amesema msimu huu wanataka kuvuka hatua hiyo wakiweka malengo ya chini ya nusu fainali.

"Wakati huu tumejipanga, tunataka kufika mbali zaidi, nusu fainali na hata fainali," aliongeza Mkwabi.

Baada ya kurejea jijini Dar es salaam leo, uongozi wa Simba uliwapa wachezaji mapumziko ya siku moja ambapo kesho wataanza maandalizi kuelekea mchezo huo ambao Mnyama anahitaji ushindi au matokeo ya sare kutinga raundi ya kwanza

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
7h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
10h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
14h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
14h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’