Mpya

Simba yarejea Dar na mkakati wa kuimaliza Mighty Wanderers

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
3d ago
Simba yarejea Dar na mkakati wa kuimaliza Mighty Wanderers

Kikosi cha Simba SC kimerejea nchini usiku wa Jumatatu, Septemba 7, 2026, kikitokea Malawi ambako juzi walijihakikishia ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mighty Wanderers katika mchezo wa kwanza wa Ligi ya Mabingwa Afrika hatua ya awali.

Mnyama amerejea nyumbani akiwa na faida ya bao moja kabla ya mchezo wa marudiano utakaopigwa Jumapili, Septemba 13, 2026, katika Uwanja wa Uhuru.

Ushindi huo wa ugenini umeiweka Simba katika nafasi nzuri ya kusonga mbele, lakini kocha mkuu wa Simba Steve Barker amesema kazi bado haijaisha. Kikosi hicho sasa kinarejea kwenye maandalizi ya mchezo wa pili kwa lengo la kupata matokeo yatakayokihakikishia tiketi ya hatua inayofuata.

Barker awataka mashabiki kuijaza Uhuru

Akizungumza baada ya kurejea nchini, Barker, amesema timu yake inahitaji kucheza kwa umakini na kuhakikisha inapata matokeo yatakayoiwezesha kufikia hatua inayofuata ya mashindano hayo.

Barker pia ametoa wito kwa mashabiki wa Simba kujitokeza kwa wingi katika Uwanja wa Uhuru Jumapili, akiamini kuwa sapoti kutoka kwa mashabiki inaweza kuwa kichocheo muhimu kwa wachezaji wakati wa kuwania ushindi.

“Tunawaomba mashabiki waje kwa wingi. Uwepo wao utawapa wachezaji hamasa kubwa katika mchezo huu muhimu,” Barker amesisitiza.

Libasse Gueye kurejea kikosini

Katika hatua nyingine, kiungo mshambuliaji Libasse Gueye amemaliza adhabu ya kadi nyekundu na atakuwa tayari kuikabili Mighty Wonderers kwenye mchezo wa marudiano.

Barker amethibitisha kuwa Barker amemaliza adhabu na atakuwa sehemu ya kikosi kitakachoikabili Mighty Wonderers Jumapili.

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
4h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
7h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
11h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
11h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
14h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’