Mlinda lango wa Simba Djibrilla Kassali jana alikuwa silaha muhimu ya Wekundu wa Msimbazi katika ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Mighty Wonderers katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya awali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika (CAFCL).
Kassali jana alidhihirisha kwa nini uamuzi wa uongozi wa Simba kumuongezea mkataba ulikuwa na maana kubwa kwani alihusika katika ushindi huo kwa asilimia 100.
Ni mara chache kusikia mlinda lango anatoa asisti, ndicho alichofanya Kassali jana kwani mpira wake mrefu ulitndewa haki na winga Anicet Oura akiifungia Simba bao muhimu ugenini ambalo liliwahakikishia Wekundu wa Msimbazi ushindi na kujiweka katika nafasi nzuri ya kufuzu raundi inayofuata kwenye michuano hiyo.
Lakini pia Kassali alifanya kazi kubwa langoni akiokoa michomo kadhaa ya hatari iliyoelekezwa kwake.
Wakati mchezo ukielekea ukiongoni, Mighty Wonderers waliongeza presha kusaka bao la kusawazisha lakini unaweza kusema kikwazo kikubwa kwao alikuwa Kassali akishirikiana vyema na safu ya ulinzi.