Mpya

Mighty Wonderers 0-1 Simba, CAFCL PR1 (FT)

Mwana Msimbazi By Mwana Msimbazi
β€’
5d ago
Mighty Wonderers 0-1 Simba, CAFCL PR1 (FT)

Klabu ya Simba SC imeanza vyema kampeni yake ya Ligi ya Mabingwa Barani Afrika (CAF Champions League) baada ya kupata ushindi muhimu wa bao 1-0 ugenini dhidi ya Mighty Wanderers ya Malawi.

Mchezo huo wa mkondo wa kwanza wa hatua ya awali ulipigwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Bingu, jijini Lilongwe, ambapo Wekundu wa Msimbazi walionyesha ukomavu mkubwa na kuondoka na mtaji mzuri wa goli la ugenini kuelekea mchezo wa marudiano.

Bao pekee na la ushindi katika mtanange huo lilipatikana kupitia kwa winga Anicet Oura.

Goli hilo lilikuja kufuatia mpango mkakati wa haraka, ambapo mlinda lango wa Simba, Djibrilla Kassali, alipiga mpira mrefu uliomkuta Oura ambaye hakufanya makosa kuwazidi ujanja mabeki wa Mighty Wanderers na kukwamisha mpira wavuni.

Baada ya goli hilo, wenyeji Mighty Wanderers walijaribu kushambulia kusaka bao la kusawazsha wakisukumwa na mashabiki wao wa nyumbani, lakini ngome ya ulinzi ya Simba na mlinda lango Kassali walikaa imara na kuzuia hatari zote hadi mwamuzi anapuliza filimbi ya mwisho.

Ushindi huu unaiweka Simba katika nafasi nzuri ya kufuzu hatua inayofuata, kwani watakuwa wenyeji katika mchezo wa marudiano utakaopigwa jijini Dar es Salaam, ambapo watahitaji sare yoyote au ushindi ili kusonga mbele.

More Stories

Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
Simba yakamilisha maandalizi dimba la Uhuru
7h ago
READ MORE β†’
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
Libasse ameweka kabatini tuzo ya kwanza ya ligi kuu msimu huu
10h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
Mighty Wonderes wawasili Dar usiku
14h ago
READ MORE β†’
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
Makgalwa ajipa muda zaidi Simba
14h ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
Magazeti ya leo Ijumaa, Septemba 11 2026
17h ago
READ MORE β†’
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
Mighty Wonderers kutua nchini leo, Simba yawaandalia dozi
1d ago
READ MORE β†’
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
Kibabage ameanza mazoezi mepesi
1d ago
READ MORE β†’
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
Chama apotezea kelele za mitandaoni, aweka msimamo
1d ago
READ MORE β†’
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
Oura anaamini huu utakuwa msimu bora kwa Simba
1d ago
READ MORE β†’
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
Magazeti ya leo Alhamisi, Septemba 10 2026
1d ago
READ MORE β†’