Kiungo fundi wa Simba Clatous Chama 'Mwamba wa Lusaka' amefichua kilichojiri nyuma ya pazia alipoondoka Simba na kujiunga na Yanga msimu wa 2024/25.
Chama amesema lilikuwa tukio ililompa wakati mgumu na alifanya jitihada za kutaka kurejesha kila kitu alichopewa na Yanga lakini haikuwezekana kwa wakati huo.
Chama amefichua hayo kwenye mahojiano maalum na Fatema Dewji.
"Ukweli ni kwamba nilijuta sana kuondoka Simba, siku niliosaini mkataba Yanga haikuwa siku nzuri sana kwangu"
"Nilimpigiaa Rais wa Yanga na kumwambia narudisha kila kitu ili nirudi Simba lakini akakataa akasema haiwezekani kwa sababu kila shabiki na kila mtu anakusubiri Yanga"
"Namshukuru Mungu sikuchukua muda mrefu pale kwa sababu sijawahi kufikiria kwenda kucheza Yanga ilitokea tu."
"Nilikuwa kwenye wakati mgumu lakini ninachoweza kusema ni kwamba nimerudi Simba na siku niliyosaini Simba nilifurahi sana na hata familia yangu ilifurahi," alisema Chama
Hata hivyo Chama alirejea Simba kwenye usajili wa dirisha dogo msimu uliopita akitokea Singida BS ambayo aliitumikia kwa miezi sita baada ya kuondoka Yanga alikocheza kwa msimu mmoja.
Chama ameanza vyema msimu huu akiwa tayari amepachika mabao matatu kwenye ligi kuu ya NBC.