After a long silence, one of the former senior leaders of Simba Crescentius Magori has scared Simba fans that happy times are about to return
Magoria who is currently an adviser to the honorary president of the Simba club Mohammed Dewji 'Mo', has said that the right way to restore the kingdom of Simba is not to fight but to cooperate
He said Mo has assured him that he will continue to cooperate with the leadership to ensure that Simba continues to dominate football in Tanzania and even Africa
Kupitia ukurasa wake wa mtandao wa Instagram, Magori ameandika ujumbe huu;
Wana-Simba naomba tutulie! Hakuna safari isiyokuwa na mabonde wala miinuko!
Safari ya Simba mpya ilianza mwaka 2018, safari ambayo mpaka sasa haijakamilika! Mategemeo ya kila Mwana-Simba ni kuwa baada ya mabadiliko ya Katiba ya mwaka huu (2024) January, Serikali itakamilisha mchakato huo hivi karibuni!
Katika kipindi hiki cha miaka 6 ya Simba mpya, Timu imepiga hatua kubwa kimaendeleo kama ifuatavyo;
1. Kutoka katika Timu isiyojulikana ni ya ngapi Afrika (unranked) mpaka namba 5 Afrika
2. Kutoka bajeti ya Tshs 3bn mpaka bajeti ya zaidi ya Tshs 20bn
3. Timu imechukua Ubingwa wa Tanzania mara 4
4. Ubingwa wa FA mara 3
5. Ngao ya jamii mara 4
6. Robo fainali ya Champions league mara 4
7. Robo fainali ya Confederation Cup mara 1
8. Ushiriki wa African Football league katika Timu 8 bora Afrika
9. Viwanja vyake vya mazoezi
10. Team ya Wanawake Simba Queens kuchukua Ubingwa mara 3
11. Team ya Wanawake Simba Queena kufika Nusu Fainali ya Champions League ya wanawake Africa
Mafanikio haya katika kipindi cha miaka 6 siyo madogo kwa namna yoyote ile! Hakuna Timu yoyote Tanzania iliyowahi kufikia mafanikio haya!
Hongera Mo Dewji, Bodi ya Simba na Menejimenti ya Klabu, Walimu, Wachezaji na kila Mwana-Simba!
Nafahamu hamu ya Wanasimba ni kurudisha Ufalme wetu hapa nyumbani na kuvuka hatua ya robo fainali kwenye michuano ya CAF!
Ndoto hizi haziwezi kufikiwa kwa mabishano, mvurugano na ugomvi bali kwa kukaa chini na kujipanga kimkakati!
Naomba niwahakikishie baada ya mazungumzo na Raisi wa Heshima wa Klabu Mohamed Dewji naomba niwatoe hofu kuwa Mo hajawahi kuiacha Simba na hataiacha Simba na kuanzia sasa atashirikiana na Uongozi kujipanga upya kurudisha heshima ya Simba na kuzidi kuimarika!
Tuachane na kelele za mitandaoni, tuwe nyuma ya Timu yetu! Simba imara inakuja!
Simba nguvu moja!